Ukraine yashambulia miundo mbinu ya nishati ya Urusi
29 Oktoba 2025
Matangazo
Katika ujumbe aliochapisha kwenye mtandao wa Telegram, gavana wa rasi ya Crimea, aliyechaguliwa na Urusi Sergei Aksyonov, amesema chombo kilichokuwa kimehifadhi mafuta mjini Simferopol kilishambuliwa na droni ya Ukraine na kushika moto.
Hata hivyo amesema hakuna vifo vilivyoripotiwa huku huduma za dharura zikifanya kazi katika eneo hilo.
Wakati huo huo, wizara ya ulinzi ya Urusi imesema kupitia ujumbe kwenye mtandao wa Telegram kwamba vikosi vyake ya ulinzi wa anga vilidungua takriban droni 100 za Ukraine usiku kucha ikiwa ni pamoja na sita kwenye eneo la Moscow na nyingine kwenye maeneo 11 ya rasi hiyo ya Crimea.