1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Ukraine yashinikiza kuwa na jeshi imara la askari 800,000

12 Desemba 2025

Ukraine inasisitiza kuwa na nguvu ya askari 800,000 katika jeshi lake chini ya pendekezo lililoboreshwa la mpango wa amani lililowasilishwa kwa Marekani.

Ukraine | Avdiivka 2024 | Wanajeshi wa Ukraine
Wanajeshi wa Ukraine wakijiandaa kurusha kombora karibu na AvdiivkaPicha: Efrem Lukatsky/AP Photo/picture alliance

Rais Volodymyr Zelensky amesema kuwa rasimu ya sasa yenye vipengele 20 imefanyiwa marekebisho ya kutosha.

Mpango wa awali wa Marekani, uliowekwa wazi mwezi Novemba, uliipangia Ukraine kikomo cha askari 600,000.

Hata hivyo, wachambuzi wameonyesha mashaka kuhusu uwezo wa Ukraine kufikia idadi hiyo. Kwa mujibu wa ofisi ya mwendesha mashtaka, kumekuwa na zaidi ya matukio 300,000 ya askari kutoroka au kutohudhuria kazini tangu uvamizi wa Urusi.

Kabla ya vita hivyo kuanza, Ukraine ilikuwa na jeshi la kudumu lenye takriban askari 290,000.

Ili kufidia upungufu wowote wa wanajeshi, Kyiv inatarajia washirika wake wa Magharibi kuchangia kuongeza nguvu ya kijeshi endapo makubaliano ya amani yatafikiwa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW