1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine yazishambuliwa Moscow, Crimea kwa droni

31 Julai 2023

Urusi imezidunguwa droni za Ukraine zilizoilenga Moscow na Rasi ya Crimea katika mashambulizi yaliyoharibu majengo mawili ya ofisi katika mji mkuu na kusitisha kwa muda shughuli katika uwanja wa ndege wa kimataifa.

Russland Moskau | Zerstörung nach Drohnenangriff
Picha: AP Photo/picture alliance

Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema droni moja iliyoilenga Moscow ilidunguliwa katika viunga vya mji huo na nyingine mbili zikaharibiwa na kuanguka katika jengo moja la ofisi mapema jana.

Kufuatia mashambulizi hayo ya droni, Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine akaonya kuwa vita vinaielemea Urusi.

Soma: Urusi kuchukua jukumu la kusafirisha nafaka barani Afrika
Urusi yaituhumu Ukraine kufanya mashambulizi ya droni Moscow

Urusi imelengwa na mfululizo wa mashambulizi ya karibuni ya droni, ikiwemo kwenye Ikulu ya Kremlin na miji ya Urusi karibu na mpaka na Ukraine -- ambayo Moscow inasema yanafanywa na Kyiv.

Wakati huo huo, maafisa wamesema Saudi Arabia mapema mwezi Agosti itakuwa mwenyeji wa mkutano wa kilele wa amani utakaoandaliwa na Ukraine ili kutafuta njia ya kuanzisha mazungumzo kuhusu vita vya Urusi nchini mwake.

Urusi haijaalikwa katika mkutano huo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW