1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Ulaya kuzindua mkakati mpya wa kuachana na nishati ya Urusi

17 Septemba 2025

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen ametangaza mpango utakaoharakisha usitishaji wa Ulaya kuagiza mafuta na nishati ya gesi kutoka Urusi.

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen
Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen.Picha: Pascal Bastien/AP Photo/picture alliance

Kiongozi huyo amesema amechukua hatua hiyo baada ya mazungumzo ya simu na Rais Donald Trump wa Marekani ambaye siku za hivi karibuni ameyarai mataifa ya Ulaya kupunguza au kusitisha kabisa uagizaji mafuta na gesi kutoka Urusi.

Bibi Von der Leyen amesema uchumi wa Urusi unaoendeshwa kwa kutegemea mapato ya nishati za visukuku ndiyo umeiwezesha Moscow kuendelea na vita nchini Ukraine.

Amearifu kwamba Umoja wa Ulaya sasa utatekeleza mkakati utakaorahisisha kuachana na ununuaji mafuta na gesi kutoka Urusi kabla ya mwaka 2028.

Vilevile Umoja huo utatangaza vikwazo ziada vya kiuchumi vitakavyozilenga sekta ya benki na nishati za Urusi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW