1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAngola

Ulaya na Afrika wakubaliana kushirikiana zaidi

26 Novemba 2025

Nchi za Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika zimesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu mwishoni mwa mkutano wao wa siku mbili katika mji mkuu wa Angola.

Angola Luanda 2025 | Wakuu wa nchi katika mkutano wa kilele wa EU-Afrika: Ursula von der Leyen, António Costa, João Goncalves Lourenço
Wakuu wa Mataifa ya Ulaya na Afrika katika mkutano wa kilele uliofanyika Luanda, Angola, 24.11.2025Picha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Tamko la pamoja lilieleza umuhimu wa kuendeleza zaidi ushirikiano na kufungua fursa mpya kwenye maeneo ya kiuchumi, biashara na uwekezaji.

Taarifa hiyo aidha ilirejelea ahadi za awali za ufadhili kwenye mabadiliko ya hali ya hewa na uimarishwaji wa nishati mbadala barani Afrika, lakini pia umuhimu wa kutatua migogoro kote ulimwenguni.

Pande zote mbili zilithibitisha tena kuzingatia demokrasia, utawala bora, utawala wa sheria, haki za binadamu na uhuru wa vyombo vya habari.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW