1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Afrika waitoa Niger katika shughuli zake zote

22 Agosti 2023

Umoja wa Afrika umeisitisha Niger katika shughuli zake zote kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya Julai 26 na kurejelea wito wake kwa viongozi wa kijeshi kumwachia rais waliyepindua Mohamed Bazoum na kurejea kwenye kambi zao

Niger Niamey | Abdourahamane Tiani
Picha: ORTN/Télé Sahel/AFP

Aidha, Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, limepitia maamuzi ya Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS ya kupeleka wanajeshi nchini Niger. Limeitaka halmashauri ya muungano wa Afrika kutathmini athari za kiuchumi, kijamii na kiusalama za uingiliaji kati kijeshi.

Jumuiya ya ECOWAS ilisema kuwa iko tayari kuwatuma wanajeshi nchini Niger, endapo juhudi za kidiplomasia zitashindikana.

ECOWAS yasema LA, kwa pendekezo la utawala wa kijeshi Niger

Umoja wa Afrika umetoa wito kwa wanachama wake wote na jumuiya ya kimataifa kujizuia na hatua yoyote inayoweza kuhalalisha utawala wa kijeshi wa Niger.

Lakini wakati huohuo umekataa uingiliaji kati wa nchi yoyote nje ya afrika.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW