1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Afrika wakutana kuzungumzia Kongo

27 Desemba 2012

Viongozi wa Umoja wa Afrika wanakutana kuzungumzia pendekezo la uwezekano wa kupeleka kikosi vya kulinda amani katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambako waasi wa M23 wanapambana na serikali.

Wapiganaji wa M23 wakiondoka Goma mwezi Disemba huku polisi wakisimama mbele yao.
Wapiganaji wa M23 wakiondoka Goma mwezi Disemba huku polisi wakisimama mbele yao.Picha: Reuters

Mkutano huo wa siku mbili unafanyika katika mjini Addis-Ababa, Ethiopia, ukiwa unahudhuriwa na viongozi wa Kanda ya Maziwa Makuu, maafisa wa Umoja wa Ulaya na wawakilishi kutoka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Ghasia zilizuka eneo hilo la mashariki mwa Kongo takriban mwezi mmoja uliopita baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Goma.

Mapema mwezi huu Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiuchumi ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ilisema iko tayari kupeleka kikosi cha kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mwandishi: Amina Abubakar
Mhariri: Josephat Charo

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW