Wanachama AU wapinga Macky Sall kugombea ukatibu mkuu UN
28 Machi 2026
Matangazo
Kulingana na taarifa, jumla ya nchi 20 wanachama wa AU, ambazo hazikutajwa zimepinga ugombea wa Macky Sall, aliyeiongoza Senegal kuanzia 2012 hadi 2024 na ambaye pia hakuungwa mkono hata na nchi yake.
Shutuma za usimamizi mbaya wa nchi dhidi ya Sall enzi za utawala wake
Ugombea wa Sall uliwasilishwa na Burundi, inayoshikilia urais wa kupokezana wa Umoja wa Afrika, lakini viongozi wa sasa ya Senegal ikiwa ni pamoja na Rais Bassirou Diomaye Faye na Waziri Mkuu Ousmane Sonko, wanawashutumu viongozi wa zamani, hasa Macky Sall, kwa usimamizi mbaya wa nchi na kuyazima kwa nguvu maandamano ya kisiasa yaliyosababisha vifo vingi vya raia.