1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Janga

Misaada ya kuwasaidia Walibya walionusurika yakusanywa

13 Septemba 2023

Umoja wa Mataifa unakusanya msaada kwaajili ya walionusurika nchini Libya kufuatia kimbunga kilichosababisha uharibifu mkubwa na kuua maelfu ya Watu.

Libyen | Überschwemmung und Hochwasser in Libyen
Picha: LIBYAN RED CRESCENT AJDABIYA/REUTERS

Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa,Stephan Dujarric, amefahamisha kwamba taasisi hiyo inashirikiana na watu ndani ya Libya na washirika wake wa kimataifa kupata msaada wa dharura wa kibinadamu utakaopelekwa katika maeneo yaliyoathirika nchini humo.

Amesema timu ya Umoja wa Mataifa iko nchini Libya na inashirikiana na maafisa wa ndani kusaidia kutathmini juhudi za kutowa msaada na  mahitaji. 

Kimbunga Daniel chaua watu zaidi ya 2,000 Libya

Kwa mujibu wa shirikisho la kimataifa la shirika la msalaba mwekundu na hilali nyekundu, Waokoaji  bado wanaendelea na operesheni za kutafuta manusura huku ikiripotiwa kwamba watu 10,000 bado hawajulikani waliko kufuatia kimbunga Daniel.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW