Umoja wa Mataifa waomba mil. 296 za kuisaidia Venezuela
9 Julai 2026
Akizungumza katika mkutano kuhusu janga hilo, Mkuu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Tom Fletcher, amesema wafadhili wameanza kujitokeza kufuatia ombi hilo baada ya ombi hilo la dola milioni 296 ili kutoa msaada wa haraka kwa watu milioni 1.3 katika kipindi cha miezi sita ijayo.
Katika hatua nyingine, serikali ya Venezuela imetoa wito wa kuachiliwa kwa mali zilizozuiwa nje ya nchi ili kusaidia kupata fedha kwa ajili ya shughuli za uokozi na ujenzi upya wa taifa hilo.
Mali hizo ni pamoja na takriban tani 30 za dhahabu ya Venezuela zinazozuiliwa chini ya vikwazo vya Uingereza.
Mahitaji ya kibinadamu yameendelea kuwa makubwa kufuatia moja ya majanga makubwa zaidi ya tetemeko la ardhi huko Amerika ya Kusini, ambalo limewaacha maelfu ya watu bila makazi na wengine wengi wakiwa bado hawajulikani walipo.