Umoja wa Mataifa waongeza makampuni 68 kwenye orodha nyeusi
26 Septemba 2025
Orodha hiyo mpya inaanganzia makampuni yanayofanya biashara zinazodhaniwa kuunga mkono makazi hayo yanayozingatiwa na wengi kuwa kinyume cha sheria kwa mujibu wa sheria za kimataifa.
Hii inajumuisha makampuni kadhaa kama ya wauzaji wa vifaa vya ujenzi pamoja na
watoa huduma za usalama, usafiri na kifedha.
Miongoni mwa makampuni yalioorodheshwa ni kundi la makampuni la Expedia lenye makao yake Marekani, Booking Holdings Inc. na Airbnb, Inc.
Nchi za makampuni yalioko kwenye orodha nyeusi
Orodha hiyo, inayojulikana rasmi kama "kanzidata ya makampuni," sasa ina makampuni 158, idadi kubwa kutoka Israel. Mengine ni kutoka Marekani, Canada, China, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Uhispania, Ureno, Uholanzi na Luxemburg.
Wakati Makampuni mpya 68 yameongezwa kwenye orodha hiyo leo Ijumaa, saba yameondolewa.
Katika awamu hii, idadi jumla ya makampuni 215 ya biashara yalifanyiwa tathmini lakini mamia zaidi yataangaziwa katika siku zijazo.