1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Mataifa waonya utatuzi mkwako wa Libya

27 Julai 2023

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya umetahadharisha dhidi ya kuchukuliwa maamuzi ya upande mmoja ya kutatua mkwamo wa kisiasa nchini humo.

Libyen | Besuch italienische Premierministerin Giorgia Meloni in Tripolis
Picha: Filippo Attili/Italian Government Press Office/ANSA/picture alliance

Hii ni baada ya mabunge mawili pinzani kupendekeza kuundwa kwa serikali mpya ya mpito, kama hatua ya mwanzo ya kuelekea kwenye uchaguzi.

Mpango huo wa Umoja wa Mataifa katika taarifa umesema, hatua za upande mmoja kama ilivyojaribiwa awali, zinaweza kuwa na athari mbaya kwa Libya na kusababisha msukosuko zaidi na machafuko.

Soma: Walinzi wa pwani ya Libya wawaokoa wahamiaji wa Kiafrika katika msitu karibu na Tunisia

Pande hizo mbili, Baraza la wawakilishi lililoko mashariki mwa nchi hiyo na Baraza Kuu la Taifa lililoko Libya, ziliunga mkono pande tofauti wakati wa mapigano kati ya mirengo ya mashariki na magharibi, ambayo tangu mwaka 2020 yametulia.

Umoja wa Mataifa unataka njia ya wazi kuelekea kufanyika uchaguzi kama sehemu ya suluhisho la kudumu kwa mzozo uliodumu kwa miaka 12 wa Libya. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW