MigogoroAfrika
Umoja wa Mataifa watoa wito wa kusitisha mapigano Sudan
30 Oktoba 2025
Matangazo
Ameyasema hayo baada ya taarifa kuwa zaidi ya watu 460 walipigwa risasi na kuuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) katika hospitali ya wajawazito kwenye mji wa El Fashir.
Hofu yazidi kutanda baada ya RSF kudhibiti El fashir
Katika tamko lake, Guterres amesema ana wasiwasi mkubwa kutokana na ongezeko la mashambulizi ya kijeshi mjini hapo siku kadhaa baada ya wanamgambo wa RSF kutangaza kuwa wameudhibiti mji huo. Mzozo kati ya wanamgambo hao na jeshi uliibuka Sudan mwezi Aprili 2023.