1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSyria

UN yafichua majaribio ya mauaji dhidi ya viongozi ya Syria

12 Februari 2026

Ripoti ya Umoja wa Mataifa imefichua kuwa Rais wa Syria pamoja na mawaziri wawili wa serikali Waziri wa Mambo ya Ndani na Waziri wa Mambo ya Nje—walilengwa katika majaribio matano ya mauaji yaliyoshindikana mwaka jana.

Syria Damascus 2025 | Rais Ahmad al‑Sharaa
Kiongozi mpya wa Syria Ahmad al‑SharaaPicha: Syrian Presidency/Handout/Anadolu/picture alliance

Ripoti hiyo iliyotolewa Jumatano na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres inaangazia kwa kina mazingira ya kiusalama nchini Syria na juhudi za makundi ya kigaidi kudhoofisha serikali mpya ya nchi hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Rais Ahmad al‑Sharaa, Waziri wa Mambo ya Ndani Anas Hasan Khattab na Waziri wa Mambo ya Nje Asaad al‑Shibani walilengwa katika majaribio matano tofauti ya mauaji. Hata hivyo, hakuna shambulio lililofanikiwa.

Majaribio hayo ya mauaji yanadaiwa kufanywa na kundi linalojiita Saraya Ansar al‑Sunnah, ambalo linatajwa kuwa kibaraka wa kundi la Dola la Kiislamu IS.

Ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa imeonya kuwa majaribio hayo ya mauaji ni ishara kwamba kundi la Dola la Kiislamu bado lina uwezo wa kupanga mashambulizi makubwa na lina nia ya kudhoofisha serikali mpya ya Syria kwa kutumia mianya ya kiusalama na mazingira ya kutokuwa na uhakika nchini humo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW