1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU kusaidia kuandaa mkutano wa kuwarejesha watoto wa Ukraine

24 Machi 2023

Rais wa Halmashauri kuu ya Ulaya Ursula von der Leyen ameahidi kusaidia maandalizi ya mkutano kwa ajili ya kuwarejesha watoto waliochukuliwa na Urusi nchini Ukraine katikati ya mzozo unaoendelea.

Belgien Geberkonferenz nach Erdbeben in der Türkei und Syrien
Picha: JOHN THYS/AFP

Von der Leyen amesema baada ya mkutano wa kilele wa viongozi wa Umoja wa Ulaya kwamba atashirikiana na waziri mkuu wa Poland Mateusz Morawiecki kuhamasisha msaada wa kimataifa wa kurejeshwa watoto hao.

Karibu watoto 16,200 walichukuliwa tangu kuanza kwa vita Februari mwaka uliopita, hii ikiwa ni kulingana na Kyiv.

Soma pia: UN: Urusi inawachukua kwa nguvu watoto wa Ukraine

Wiki iliyopita Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu, ICC ilitoa waranti wa kukamatwa rais Vladimir Putin wa Urusi ikimshutumu kwa makosa ya uhalifu wa kivita ikisema alisimamia mchakato wa kuwachukua watoto hao.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW