1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaUlaya

Umoja wa Ulaya na India waingia makubaliano ya biashara huru

27 Januari 2026

Umoja wa Ulaya na India wamefikia makubaliano ya kihistoria ya biashara huria, hatua inayoimarisha zaidi uhusiano kati ya pande hizo zenye uchumi mkubwa duniani.

India New-Delhi 2026 | Von der Leyen, Costa na Modi
Rais wa Baraza la Ulaya Antonio Costa, Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi wakishikana mikono kabla ya mkutano wao huko New Delhi, India, Januari 27, 2026.Picha: Altaf Hussain/REUTERS

Rais wa Halmashauri Kuu ya Ulaya Ursula von der Leyen pamoja na Waziri Mkuu wa India wamesema hayo mapema leo baada ya mkutano wa kilele kati ya Ulaya na India mjini New Delhi.

Amesema "Sekta ya uzalishaji itapata msukumo mkubwa kutokana na makubaliano haya ya biashara na Umoja wa Ulaya, na sekta ya huduma pia itaimarika. Mkataba wa Biashara Huria utaongeza imani ya kila mwekezaji na mfanyabiashara kuwekeza nchini India."

Bi von der Leyen amesema wameunda ukanda wa biashara huria itakayokutanisha watu bilioni 2, huku pande zote mbili zikitarajia kunufaika.

Chini ya makubaliano hayo, India inataraji kupunguza ushuru wa magari yanayoingizwa kutoka nje kutoka asilimia 110 hadi asilimia 10 na pia itaondoa ushuru wa vipuri vya magari katika kipindi cha miaka mitano hadi 10.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW