1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya umeiwekea vikwazo Myanmar

22 Februari 2022

Umoja wa Ulaya umewawekea vikwazo maafisa waandamizi wa Myanmar na biashara ya mafuta na gesi vinavyomilikiwa na serikali na kuisiadia serikali ya kijeshi ambayo iliiondoa madarakani ya kiraia mwaka mmoja uliopita.

Myanmar | Unterstützer der Militärregierung
Picha: AP Photo/picture alliance

Mataifa wanachama ya umoja huo yamezuia mali na marufuku ya kusafiri kwa maafisa 22 na kadhalika kuzua makampuni manne, yakiwemo yanayomilikiwa na serikali pamoja na watu binafsi.

Miongoni mwa yaliwekewa vikwazo ni pamoja na yale yanayomilikiwa na serikali kama kampuni ya mafuta ya Myanmar lijulikanalo kama Myanma Oil na ya gesi, Enterprise (MOGE)  yenye ubia wa pamoja. Vikwazo dhidi ya MOGE  kunatokana na kampeni ya muda mrefu ya makundi ya haki za binaadamu ya Myanmar na kwengineko duniani, ambayo yalikuwa yanasema hatua hiyo inaweza kuuondolea utawala wa kijeshi kupata kipato cha kujiendesha kwake.

Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya Myanmra asilimia 50 za mapato yake yatokanayo na fedha za kigeni yanatokana na rasilimali ya gesi, ambapo kampuni MOGE inakadiriwa kuliingizia taifa hilo kiasi cha dola bilioni 1.5 kwa mwaka 2021-2022. Katika duru za awali vikwazo vya Marekani na Umoja wa Ulaya  dhidi ya Myanmar havikuigusa sekta ya gesi.

Wasiwasi wa hali kuendelea kuwa mbaya nchini Myanmar

Katika taarifa yake makao makuu ya Umoja wa Ulaya imesema ina wasiwasi mkubwa na hali ya kuendelea kwa machafuko nchini Myanmar na kuzuka na athari zake kikanda. Tangu kutokee mapinduzi ya kijeshi kwa mfululizo hali imeendelea kuzorota na kuwa mbaya zaidi.

Kiongozi wa kijeshi wa Myanmar Min Aung Hlaing Picha: Sefa Karacan/AA/picture alliance

John Sifton, ambae ni mkurugenzi wa utetezi wa kwa bara la  Asia wa shirika la  Human Rights Watch, ameonekana akipongeza uamuzi wa Umoja wa Ulaya kwa kusema vikwazo dhidi ya MOGE vilikuwa na umuhimu hasa ikizingatiwa jinsi mapato ya kampuni yalivyokuwa muhimu kwa wanajeshi.

Wimbi kubwa la maandamano ya amani nchini Myanmar lilitokana na mapinduzi ya Februari Mosi, 2021, dhidi ya kiongozi aliyechaguliwa kidemokrasia Aung San Suu Kyi. Kupingwa kwa jeshi kuliongezea baada ya ukandamizaji dhidi ya raia katika maandamano hayo.

Taifa hilo kwa sasa linakalibiliwa na uasi katika kiwango ambacho wataalam wanasema kama lipo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Takribani watu 1,500 wameuwawa kwa kuteswa au kuuwawa katika vurugu, ambapo mashambulizi mengi yametokea katika maeneo ya vijinini yakiwemo ya anga.

Hadi wakati huu Umoja wa Ulaya wenye mataifa 27, imeweka vikwazo kwa jumla ya watu 65 na taasisi 10, ambazo zinaweza kuwa mashirika, makampuni, vyama au benki.

Chanzo: AP

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW