1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU yahaha kukwepa ushuru wa Trump kuhusu Greenland

19 Januari 2026

Mabalozi wa Umoja wa Ulaya wanazidisha juhudi za kumzuwia Rais Donald Trump wa Marekani asiwawekee washirika wa Ulaya ushuru mkubwa, wakati wakijitayarisha na hatua za kulipiza kisasi endapo ushuru utaongezwa.

Greenland Nuuk 2026 | Waziri Mkuu Jens-Frederik Nielsen
Maandamano mjini Nuuk kupinga kitisho cha Rais Donald Trump wa Marekani kutaka kukichukuwa kisiwa cha Greenland.Picha: Evgeniy Maloletka/AP Photo/picture alliance

Siku ya Jumamosi (Januari 17), Trump alitishia kuyapandishia ushuru mataifa sita ya Umoja wa Ulaya pamoja na Norway na Uingereza, hadi pale Marekani itakaporuhusiwa kukinunuwa kisiwa cha Greenland

Mataifa hayo ni Denmark, Sweden, Ufaransa, Ujerumani, Uholanzi na Finland. Mataifa makubwa ya Umoja wa Ulaya yamekiita kitisho hicho cha Trump kuwa ni ghiliba.

Viongozi wakuu wa Umoja huo wanatazamiwa kukutana mjini Brussels kwa mkutano wa dharura wa kilele hapo Alkhamis kujadili hatua za kuchukuwa.

Mojawapo ya hatua hizo ni ushuru wa euro bilioni 93 kwa bidhaa za Marekani unaoweza kuanza kazi tarehe 6 Februari baada ya kusitishwa kwa miezi sita.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW