1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya wahimiza diplomasia mzozo wa Hormuz

17 Machi 2026

Umoja wa Ulaya unaamini njia za kidiplomasia zinapaswa kupewa kipaumbele kutatua mvutano kuhusu mlango bahari wa Hormuz

Njia ya mlango bahari ya Hormuz imefungwa na Iran ambayo imeaapa meli yoyote ya adui itakayopita itaripuliwa
Njia ya mlango bahari ya Hormuz imefungwa na Iran ambayo imeaapa meli yoyote ya adui itakayopita itaripuliwaPicha: Francis Mascarenhas/REUTERS

Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas amesema Umoja wa Ulaya unataka njia za kidiplomasia zitumike kutafuta mwafaka wa  kuufungua mlango bahari wa Hormuz.

Kauli hiyo imetolewa baada ya miito ya rais Donald Trump wa Marekani ya kuwataka washirika wake wapeleke meli za kivita kwenye eneo hilo kutowa ulinzi kufuatia vita dhidi ya Iran.

Washirika wa Marekani wakataa ombi la Trump la kupeleka Meli zao Hormuz

Kallas ameweka wazi kwamba hakuna anayetaka kuhatarisha maisha ya watu wake katika mlango bahari wa Hormuz na kwa hivyo kuepusha mgogoro wa chakula, mbolea na nishati, njia za kidiplomasia zinapaswa kutumika kuutatua mgogoro huo.

Rais Trump ameyatishia mataifa ya jumuiya ya NATO kwamba mustakabali wao utakuwa mbaya ikiwa yatakataa kupeleka meli za kijeshi kwenye mlango bahari wa Hormuz.Hezbollah

Ujerumani na mataifa kadhaa ikiwemo Japan, Poland,Uhispania, Sweden na Australia yamekataa wito wa Trump.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW