1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Mamia ya watu huenda waliuawa El- Fasher

31 Oktoba 2025

Mamia ya raia wa Sudan na wapiganaji wasio na silaha huenda wameuawa wakati kundi la RSF lilipouteka mji wa El- Fasher. Haya yamesemwa leo na Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa.

Sudan El-Fasher 2025 | RSF
Wapiganaji wa RSF wakimkata mwenzao anayejulikana kama Abu Lulu kwa madai ya unyanyasajiPicha: Rapid Support Forces (RSF)/AFP

Wakati wa mkutano na waandishi wa habari hii leo mjini Geneva, msemaji wa Ofisi ya Haki ya Binadamu ya Umoja wa Mataifa amesema wanakadiria idadi ya vifo vya raia na wale waliotekwa wakati wa uvamizi huo wa RSF na njia za kutoka mjini huo huenda ikafikia mamia na kuelezea ushahidi wa mauaji makubwa ya kiholela.

Kuna ushahidi wa kubakwa kwa watu wasioungua wanawake 25

Magango amesema ofisi hiyo imepokea ushuhuda kutoka kwa wafanyakazi wa mashirika ya misaada kwamba watu wasiopungua wanawake 25 walibakwa na magenge wakati wapiganaji wa RSF walipoingia kwenye kambi za watu waliopoteza makazi yao karibu na chuo kimoja kikuu.

Pia amewaambia waandishi wa habari kwamba mashuhuda wamethibitisha kuwa wapiganaji wa RSF waliwachagua wanawake na wasichana na kuwabaka kwa makundi wakiwa wamewaelekezea bunduki, na kulazimisha takriban familia 100 zilizopoteza makazi kuondoka eneo .