UN: Takriban watu milioni 4 wapoteza makao eneo la Sahel
11 Oktoba 2025
Matangazo
Mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi katika kanda ya Afrika Magharibi na Kati Abdouraouf Gnon-Konde, amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva Uswisi kwamba waliopoteza makaazi yao wanatokea Burkina Faso, Mali, Niger na nchi jirani ya hizo, na idadi yao inakaribia theluthi mbili zaidi, ikilinganishwa na idadi ya miaka mitano iliyopita.
Gnon-Konde amesema hali hii inaashiria ukosefu wa usalama, upatikanaji mdogo wa huduma na njia za kukidhi maisha, pamoja na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.