1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Tani 170,000 za msaada zinasubiri kuingia Gaza

9 Oktoba 2025

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kiutu, OCHA imesema takribani tani 170,000 za misaada zimeandaliwa na zinasubiri kupelekwa katika Ukanda wa Gaza.

Ägypten Grenzübergang Rafah | Hilfgüter Werden in den Gazastreifen gebracht
Picha: Ahmed Gomaa/Xinhua/IMAGO

Msemaji wa OCHA, ameyasema hayo Alhamisi baada ya Israel na Hamas kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano katika awamu ya kwanza ya mpango wa amani wa Gaza.

Amesema mara tu maafisa wa Israel watakapotoa idhini, misaada hiyo inaweza kupelekwa kwa watu wenye uhitaji.

Amesema misaada hiyo ni pamoja na chakula, dawa, mahema na misaada mingine inayohitajika haraka.

Asilimia 45 ya magari ya misaada imezuiwa

Mapema wiki hii, OCHA ilisema maafisa wa Israel ama hawajaidhinisha au wamezuia asilimia 45 ya magari yake ya misaada yaliyoorodheshwa tangu vita vilipoanza Oktoba, 2023.

Amesema ili kutoa msaada kwa raia, OCHA inahitaji maeneo ya kuvukia ya mipakani yawe wazi, usalama kwa wafanyakazi wa mashirika ya misaada uhakikishwe, na wale wenye uhitahaji waweze kuhama kwa usalama.

Wakati huo huo, Israel imesema usitishaji mapigano utaanza kutekelezwa ndani ya saa 24 baada ya mkutano wa baraza la mawaziri la usalama.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW