1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yamteua Sigrid Kaag kama mratibu mpya wa misaada Gaza

27 Desemba 2023

Naibu waziri Mkuu wa Uholazi Sigrid Kaag, ambaye pia ni mtaalamu wa Mashariki ya Kati ameteuliwa kuwa mratibu wa Umoja wa Mataifa kusimamia misaada ya kibinaadamu kuingia katika eneo linalokumbwa na vita la Gaza.

Diplomasia l Mratibu wa Umoja wa Mataifa kusimamia misaada kuingia Gaza Sigrid Kaag
Naibu waziri Mkuu wa Uholazi Sigrid Kaag ambae amechaguliwa kuwa Mratibu wa Umoja wa Mataifa kusimamia misaada kuingia GazaPicha: Sem Van Der Wal/ANP/dpa/picture alliance

Tangazo hilo lililotolea na katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres limekuja baada ya Baraza la Usalama la umoja huo, kupitisha azimio lililompa nafasi ya kumteua mratibu maalum kwaajili ya Gaza ambako zaidi ya watu milioni 2 wanauhitaji mkubwa wa dharura wa maji, chakula na dawa. Kaag anatarajiwa kuanza kuratibu majukumu yake Tarehe 8 Januari

Soma pia:Hamas yakataa pendekezo la kusitisha mapigano kwa muda

Watu zaidi ya 20,000 wakiwemo watoto 8000 wameuwawa tangu kuanza kwa vita kati ya Israel na Hamasmnamo Oktoba 7.  Marekani, Umoja wa Ulaya na nchi kadhaa za Magharibi zimeliorodhesha kundi la Hamas kama kundi la kigaidi. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW