1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yarefusha muda wa kikosi chake cha amani huko Abyei

15 Novemba 2025

Baraza la Usalama la UN limepigia kura azimio la kuongeza muda wa ujumbe wa kulinda amani katika eneo la Abyei lenye utajiri wa mafuta na linalozozaniwa kati ya Sudan na Sudan Kusini.

Maafisa wa Kikosi cha usalama cha Umoja wa Mataifa UNMIS wakitembea katikati ya Abyei
Biashara na nyumba zateketea katikati mwa Abyei mnamo Mei 28, 2011Picha: Stuart Price/Unmis Photo/dpa/picture alliance

Wanachama 12 waliunga mkono azimio hilo huku Urusi, China na Pakistan zikikosa kushiriki.  Azimio hilo la kuongeza muda kwa kikosi hicho cha kulinda amani kinachojulikana kama UNISFA lilitayarishwa na Marekani ili kuongeza muda wa ujumbe huo hadi Novemba 2026.

Linasema kuwa Baraza la Usalama lina "nia" ya kurefusha zaidi muda wa ujumbe huo haswa kwa kuunda jeshi la polisi la pamoja la Abyei na kumaliza kabisa shughuli za kijeshi kama ilivyokubaliwa na pande hizo mbili mnamo mwaka 2011.

Azimio hilo pia linamtaka Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuwasilisha ripoti ifikapo Agosti 2026, kuhusu maendeleo yoyote yatakayofanywa na nchi hizo mbili na kutathmini kuhusu kitakachotokea ikiwa kikosi hicho kitapunguzwa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW