1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yasema haina mabilioni ya dola kulisha wenye njaa duniani

18 Novemba 2025

Shirika la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, limeonya kuwa kupunguzwa kwa ufadhili kunamaanisha kuwa litakumbwa na changamoto katika kulisha hata theluthi moja ya watu milioni 318 wanaokabiliwa na njaa kali mnamo 2026.

Sudan Kusini  Bentiu 2025 | Chakula cha msaada
Wakimbizi katika kambi ya Bentiu nchini Sudan Kusini wapokea chakula cha msaada kutoka shirika la WFP mnamo Novemba 4, 2025Picha: Rian Cope/AFP

Katika taarifa yake, shirika hilo limesema kupungua kwa ufadhili kwa huduma za kibinadamu duniani kunalilazimisha shirika hilo kutoa kipaumbele cha msaada wa chakula kwa takribani theluthi moja ya wale wanaohitaji na kuwalenga watu milioni 110 wanaokabiliwa na hatari zaidi.

WFP inahofia kiwango kidogo zaidi cha ufadhili

Pia limekadiria kwamba hatua hiyo italigharimu shirika hilo dola bilioni 13, lakini likaonya kuwa "makisio ya sasa ya ufadhili" yanaonyesha WFP inaweza kupokea nusu tu ya kiasi hicho.

WFP imesema watu milioni 318 wanaokabiliwa na njaa kali ni zaidi ya mara mbili ya idadi iliyorekodiwa mwaka 2019, huku mizozo, hali mbaya ya hewa na kuyumba kwa uchumi kukiwaathiri.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW