MigogoroKimataifa
UN yatahadharisha tabia ya kutumia mabavu kutatua mizozo
28 Februari 2026
Matangazo
Volker Turk ameliambia Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa hapo jana mjini Geneva kuwa kunashuhudiwa "mparaganyiko duniani" kufuatia kitendo cha kuchukulia kawaida matumizi ya nguvu, huku akitolea mifano mizozo ya Sudan, Ukraine na maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu.
Turk amesema idadi ya migogoro inayohusisha silaha imeongezeka maradufu tangu mwaka 2010 na kufikia karibu migogoro 60, huku akitamatisha kuwa kwa sasa dunia inazidi kuwa eneo hatari zaidi.