Janga
UN yataka haki itendeke baada ya shule ya Iran kushambuliwa
27 Machi 2026
Matangazo
Mkuu wa Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa, Volker Turk, amesema kushambuliwa kwa shule hiyo ya msingi ya Shajareh Tayyebeh, kulibainisha ukatili usioelezeka dhidi ya watoto, na kwamba lazima kuwe na uwajibikaji kwa waliohusika.
Katika mkutano wa Baraza hilo mjini Geneva, Turk alisema mvutano ulioko kwa sasa dhidi ya mataifa yaliyovitani, hauwezi kusuluhishwa kwa mauaji ya wanafunzi.
Amesema mauaji hayo yamefungua dirisha kubwa la hofu duniani na kwamba haki lazima itendeke.
Turk ameitolea mwito Marekani kukamilisha haraka uchunguzi wa shambulizi dhidi ya shule hiyo akisema matokeo yake ni lazima yatangazwe hadharani.