1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres ataka suluhu ya Mataifa mawili Israel na Palestina

21 Januari 2024

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amerejelea wito wake wa kutaka kupatikana suluhisho la Mataifa mawili katika mzozo wa Israel na Hamas, huku Waziri Mkuu wa Israel akiendelea kupinga wito huo.

 Antonio Guterres | Umoja wa Mataifa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres Picha: Gian Ehrenzeller/KEYSTONE/picture alliance

Guterres alisema jana Jumamosi kwamba haki ya wapalestina kuwa na taifa lao ni lazima itambuliwe na kila mmoja.

Akizungumza mjini Kampala katika mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya nchi zisizofungamana na upande wowote, Guterres alisema hatua ya kukataa kutambuwa haki hiyo kwa watu wa palestina haitokubalika. 

Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amesema kukataliwa suluhu ya mataifa mawili kunaendeleza mgogoro uliopo ambao umekuwa tishio kwa usalama na amani ya dunia na kuchangia ubaguzi na kuendeleza misimamo mikali kila sehemu. 

Nchi za kiarabu na Ulaya zapigia debe suluhisho la mataifa mawili mzozo wa Mashariki ya Kati


Amerejelea pia wito wake wa kutaka kusimamishwa kwa mapigano kati ya Israel na Hamas katika Ukanda wa Gaza. 

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Nentanyahu ameendelea kukataa mpango wa suluhu ya Mataifa mawili katika mgogoro huo wa Israel na Palestina. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW