1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

UN yazituhumu Urusi na Ukraine kwa kuwauwa wafungwa

Angela Mdungu
25 Machi 2023

Umoja wa Mataifa umesema una hofu kubwa ya kile ilichosema kuwa ni kuuwawaa kwa wafungwa wa kivita kunakofanywa na wanajeshi wa Urusi na Ukraine katika uwanja wa mapambano.

Gefangenenaustausch Russland Ukraine
Picha: RUSSIAN DEFENCE MINISTRY/ REUTERS

Tuhuma hizo zimetolewa baada ya Ukraine kudai kuwa wanajeshi wa Urusi walimuuwa mpiganaji wa Ukraine aliyechukuliwa video akisema "Utukufu kwa Ukraine" kabla ya kupigwa risasi.

Mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaofuatilia haki za binadamu nchini Ukraine Matilda Bogner, amesema shirika lake limerekodi mauaji kutoka pande zote mbili.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana Ijumaa, Bogner alisema wana hofu pia kuhusu taarifa za kuuwawa kwa wafungwa 25 wa Urusi uliofanywa na majeshi ya Ukraine.

Katika taarifa tofauti, wizara ya mambo ya kigeni ya Ukraine, iliushukuru Umoja wa Mataifa kwa kazi yao, lakini ilisisitiza kuwa inatarajia umoja huo utajiepusha na hatua zozote zinazoweza kutafsiriwa kuwa ni sawa na "kufananisha muathiriwa na  mchokozi."

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW