1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Wakimbizi 900 wa Rohingya wamekufa, hawajulikani waliko

17 Aprili 2026

Umoja wa Mataifa umeripoti kuwa zaidi ya wakimbizi 900 wa jamii ya walio wachache ya Rohingya walipotea au kufa maji katika Bahari ya Andaman na Ghuba ya Bengal mwaka 2025.

Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya Wakimbizi 900 wa Rohingya walikufa maji au walipotea mwaka 2025
Wakimbizi wa jamii ya Rohingya Picha: AFP

Msemaji wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR  Babar Baloch amefafanua kuwa kati ya zaidi ya wakimbizi 6,500 waliojaribu kuvuka baharini, mmoja kati ya saba hajulikani aliko au alikufa maji. Amesema takwimu hizo zinaonesha idadi kubwa zaidi ya vifo kwa wakimbizi na wahamiaji wanaosafiri kwa njia ya bahari kote duniani.

Wengi wa wakimbizi wa Rohingya wanakimbia hali duni, unyanyasaji

Wakimbizi wengi wa Rohingya hutoka katika kambi kubwa za Cox's Bazar nchini Bangladesh, ambako zaidi ya milioni moja wanaishi katika hali duni. Wengi wao walikimbia kutoka jimbo la Rakhine la Myanmar ambalo linakabiliwa na mapigano kati ya jeshi na waasi wa Arakan. Huko, wamekuwa wakikabiliwa na unyanyasaji na kunyimwa uraia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW