1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Zaidi ya wanawake, wasichana 38,000 waliuwawa vita vya Gaza

17 Aprili 2026

Umoja wa Mataifa umebainisha kuwa zaidi ya wanawake na wasichana 38,000 waliuwawa wakati wa vita vya Israel dhidi ya kundi la Hamas kwenye Ukanda wa Gaza kufikia mwishoni mwa mwaka 2025.

Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya wanawake na watoto 38,000 waliuwawa katika vita Ukanda wa Gaza
Ukanda wa GazaPicha: Abdalhkem Abu Riash/Anadolu Agency/IMAGO

Idadi hiyo ni sawa na nusu ya idadi ya vifo 71,000 viivyotangazwa na Wizara ya Afya ya  Msemaji wa Shirika la Wanawake la Umoja wa Mataifa Sofia Calltorp amesema kando ya vifo hivyo, karibu wanawake na wasichana 11,000 walipata majeraha makubwa ambayo yamewafanya waishi na ulemavu maisha yao yote.

Ugumu wa maisha wazidi kuwaumiza wanawake

Calltorp ameongeza kuwa vita vimebadilisha maisha ya familia za Wapalestina ambapo maelfu ya wanawake ambao waume zao waliuwawa wanapambana kuziendesha familia bila kipato msaada wala huduma muhimu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW