UNICEF: Watoto Kongo wakabiliwa na hatari ya unyanyasaji
30 Desemba 2025
Matangazo
Hayo yameelezwa leo katika ripoti iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia Watoto (UNICEF), ripoti iliyoongeza kuwa miaka thelathini ya mzozo mashariki mwa Kongo ni moja ya sababu kubwa ya madhila hayo kwa watoto yanayochagizwa na mifumo dhaifu ya ulinzi na uwajibikaji mdogo wa kisheria.
Lakini pia UNICEF imeripoti vitendo vya unyanyasaji mkubwa wa kingono hata nje ya maeneo yenye migogoro na kwamba licha ya miongo kadhaa ya juhudi endelevu za kitaifa na kimataifa, ukiukwaji huo unaendelea katika viwango vya kutisha kote nchini Kongo.