1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Upigaji kura wafanyika kwa amani Nepal baada ya mapinduzi

5 Machi 2026

Zoezi la kupiga kura linaendelea kwa amani nchini Nepal katika uchaguzi wa kwanza mkuu nchini humo tangu maandamano yaliyoongozwa na vijana kuipelekea serikali kuachia mamlaka mnamo Septemba.

Wapiga kura wakipanga mstari kaika kituo cha kupigia kura Kathmandu
Wapiga kura wakipanga mstari kaika kituo cha kupigia kura KathmanduPicha: Ritesh Shukla/Getty Images

Maafisa wa usalama wamepiga doria na kuvilinda vituo vya kupigiakura katika taifa hilo lililoko katika milima ya Himalaya, huku wapiga kura wakipanga mistari kupiga kura zao.

Kulingana na maafisa, kampeni zilifanyika kwa amani kuelekea Alhamis ya leo ya upigaji kura. Mamlaka zimepiga uendeshaji wa magari barabarani pamoja na kufanyika mikutano ya kisiasa.

Kulingana na tume ya uchaguzi nchini humo, yapata watu milioni 19 kati ya idadi jumla ya watu milioni 30 nchini humo wamejiandikisha kupiga kura.

Karibu Wanepal milioni 3 wanaishi nje ya nchi ila hawatoweza kushiriki upigaji kura.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW