1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan Kusini

Upinzani wapuuza wito wa mazungumzo ya amani Sudan Kusini

18 Julai 2025

Chama kikuu cha upinzani nchini Sudan Kusini kimekataa wito wa Rais Salva Kiir wa kuanzisha mazungumzo ya kitaifa ili kuzuia nchi hiyo kurejea katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Sudan Kusini- Salva Kiir na Riek Machar
Hali nchini Sudan Kusini inaendelea kuwa ya wasiwasi baada ya Makamu wa Rais Riek Machar kuwekwa chini ya kizuizi cha nyumbani.Picha: Peter Louis Gume/AFP

Pal Mai Deng, msemaji wa chama cha upinzani SPLM-IO, amesema Rais Kiir anapaswa kwanza kuwaachilia viongozi wa kisiasa na kijeshi walioko gerezani ili kudhihirisha nia ya kweli kuhusu mazungumzo hayo.

Kauli ya Rais Kiir imejiri katika hotuba yake wakati wa kufungua tena bunge, akisisitiza haja ya umoja na maridhiano ya kitaifa, akisema "milango ya amani bado iko wazi.”

Hali nchini Sudan Kusini inaendelea kuwa ya wasiwasi baada ya Makamu wa Rais Riek Machar— mpinzani wa zamani wa Kiir — kuwekwa chini ya kizuizi cha nyumbani kufuatia shambulio dhidi ya vituo vya jeshi mwezi Machi. Wanachama wengi wa chama cha upinzani wamekimbia nchi kwa hofu ya kukamatwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW