1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi huenda ilihusika na hujuma za Kakhovka

18 Juni 2023

Jarida la New York Times la nchini Marekani limesema kuna ushahidi unaopendekeza kwamba Urusi ilihusika na shambulizi la bwawa kubwa la Kakhovka, lililopo katika eneo linalodhibitiwa na Urusi nchini Ukraine.

Luftaufnahme einer durch den Bruch des Nova Kakhovka-Dammes gefluteten Landschaft bei Kherson
Picha: Inna Varenytsia/REUTERS

Jarida hilo lililowanukuu mafundi na wataalamu wa milipuko liliripoti siku ya Ijumaa kwamba uchunguzi wake umebaini ushahidi uliopo unapendekeza, mlipuko huo ulitokea ndani.

Soma Zaidi:Maafisa wa Ukraine wasema athari za kupasuka kwa bwawa la Kakhova zitaendelea 

Katika nyakati tofauti, timu za kimataifa za kisheria zinazowasaidia wanasheria wa Ukraine katia uchunguzi zimesema katika ripoti za awali za utafiti kwamba kuna uwezekano mkubwa kisa hicho katika eneo la Kherson kilisababishwa na milipuko iliyotegwa na Urusi.

Urusi imekuwa ikiituhumu Kyiv kwa kuhujumu bwawa hilo la kuzalisha umeme ili pamoja na mambo mengine, kuharibu chanzo muhimu cha maji katika rasi ya Crimea.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW