1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi kujadili hatma ya askari wake Nagorno-Karabakh

11 Oktoba 2023

Urusi leo imesema itajadili na Azerbaijan mustakabali wa walinda amani wake huko Nagorno-Karabakh, wiki chache baada ya Baku kuliteka tena eneo hilo lililojitenga ambalo lilikuwa linaendeshwa na Waarmenia.

Rais wa Urusi Vladimir Putin
Rais wa Urusi Vladimir PutinPicha: Grigory Sysoyev/AFP

Hatua ya Urusi kutoingilia kati uvamizi wa haraka wa Azerbaijan, umeipelekea Armenia ihisi kutoungwa mkono na rafiki yake Moscow.

Sehemu kubwa ya Waarmenia 120,000waliokuwa Nagorno-Karabakhkwa sasa wamekimbilia Armenia.

Soma pia:Azerbaijan yamkamata rais wa zamani wa Nagorno-Karabakh

Azerbaijan ililiteka tena eneo hilo kufuatia zuio la miezi tisa la usambazaji chakula na nishati kuingia Nagorno-Karabakh na walinda amani wa Urusihawakuchukua hatua yoyote ile kufanya hali kuwa bora. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW