1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

Urusi na China zafanya luteka za pamoja za kijeshi

21 Julai 2023

Urusi imeanza luteka ya pamoja ya kijeshi na China katika Bahari ya Japan, wakati ushirikiano wa kijeshi baina ya mataifa hayo mawili ukizidi kuimarika.

Marine-Manöver Beteiligung Russland China und Iran
Picha: Russian Defense Ministry/AP/picture alliance

Wizara ya ulinzi ya Urusi, imesema lengo mahususi la luteka hizo zinazohusisha ndege 30 za majeshi ya wanamaji na zitakazofanyika hadi Jumapili ni kuimarisha ushirikiano wa majeshi yao ya majini na kudumisha utulivu na amani katika ukanda wa Asia-Pasifiki.

Soma pia: Urusi na China zasaini mikataba ya kiuchumi

Luteka hizo zitahusisha makabiliano ya majini na baharini na hewani, wizara hiyo imesema na kuongeza kuwa kuna mipango pia ya kufanya luteka za pamoja za ufyatuaji wa mizinga.

Katika hatua nyingine, Urusi imefanya mazoezi ya kijeshi kaskazinimagharibi mwa Bahari Nyeusi, wizara hiyo imesema hii leo, siku chache baada ya ikulu ya Kremlin kusema kuwa itazingatia meli zinazokwenda Ukraine kupitia njia hiyo ya baharini kuwa kiticho cha kijeshi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW