1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Ukraine yasema kuwa tayari kwa makubaliano ya kumaliza vita

8 Aprili 2026

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema nchi yake iko tayari kwa mpango wa usitishaji mapigano na Urusi, huku akimtolea wito rais wa Marekani Donald Trump kuishinikiza Moscow kusitisha uvamizi wake.

Ukraine Butscha 2026 | Selenskyj spricht auf dem Butscha-Gipfel zur Presse
Picha: Tetiana Dzhafarova/AFP

Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Andriy Sybiha amesema makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na Iran yanaonyesha mafanikio ya "uamuzi" wa Marekani na kuitaka Washington isiupuuze mzozo wa Ukraine.

Hayo yakiripotiwa, Urusi na Ukraine zimeendelea kushambuliana usiku kucha,  huku shambulizi la droni la Moscow likisababisha uharibifu mkubwa kwenye bandari ya mji wa Izmail iliyopo kwenye mto Danube kusini-magharibi mwa Ukraine.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW