1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi na Ukraine zashambuliana, watu wawili wauwawa

20 Machi 2026

Mashambulizi ya Urusi na Ukraine yamewaua watu wawili kila upande wa mpaka leo Ijumaa, huku meli mbili za mizigo zenye bendera ya kigeni zilizojaa nafaka zikishambuliwa kusini mwa Ukraine.

Magari ya uokozi yakufanya operesheni ya uokoaji baada ya shambulizi la droni la Urusi
Magari ya uokozi yakufanya operesheni ya uokoaji baada ya shambulizi la droni la UrusiPicha: State Emergency Service of Ukraine in Odesa region/Handout/REUTERS

Maafisa wametangaza kuwa mashambulizi ya usiku kucha kat ya Ukraine na Urusi yalitokea wakati rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alipotangaza kwamba wapatanishi kutoka Kyiv walikuwa wakisafiri kwenda Marekani kwa lengo la kuanzisha tena mazungumzo ya pande tatu na Urusi.

Mkuu wa eneo la kusini mwa Ukraine la Zaporizhzhia alisema mashambulizi ya Urusi huko yalimuua mwanamke wa miaka 30 na kumjeruhi mvulana mmoja, 10, na mwanamume mmoja, 48.

Jeshi la anga la Ukraine lilitangaza kwamba Urusi ilikuwa imeshambulia nchi hiyo kwa kutumia ndege zisizo na rubani 156 na kwamba mifumo ya ulinzi wa anga ilikuwa imeziangusha 133 kati yao.

Shambulio la Urusi lililenga maeneo kadhaa ikiwa ni pamoja na mji wa bandari wa kusini wa Odesa ambapo maafisa walisema meli mbili za mizigo zilizojaa nafaka zilikuwa zimeharibiwa, na kwamba wafanyakazi wawili walijeruhiwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW