1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Urusi: Ujerumani inazidi kujiingiza kwenye vita vya Ukraine

2 Mei 2023

Serikali ya Urusi imesema hii leo kwamba Ujerumani inazidi kujihusisha na vita nchini Ukraine siku hadi siku.

Pichani ni wanajeshi wa Ukraine wakiwa juu ya kifaru, karibu na mkoa wa Donesk.
Mashambulizi ya Urusi nchini Ukraine tayari yamesababisha maafa makubwa ikiwa ni pamoja na uharibifu wa miundombinu ya Ukraine. Picha: Libkos/AP Photo/picture alliance

Kulingana na Moscow, serikali mjini Berlin haina namna yoyote ya  kuhakikisha kwamba silaha ilizoipatia Ukraine hazitotumika dhidi ya maeneo ya Urusi.

Hayo yameelezwa na msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov ambaye amesema silaha za Ujerumani zilizopelekwa Ukraine tayari zinatumiwa kwenye vita katika eneo la Donbas,ambalo Urusi imeshalitangaza kuwa eneo lake.

Kwa upande mwingine serikali ya Ukraine mjini Kiev imesema Urusi imebadili mbinu katika vita nchini humo na sasa imeanza  kuyalenga kwa makusudi maeneo ya makaazi ya watu katika mashambulizi yake ya anga.

Mshauri wa rais Volodymry Zelensky, Mykhailo Podolyak amesema hakuna shaka kwamba Urusi inafanya mashambulizi dhidi ya makaazi ya raia au maeneo yenye makaazi mengi ya raia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW