MigogoroUlaya
Urusi yaanzisha tena mashambulizi dhidi ya Ukraine
21 Aprili 2025
Matangazo
Hata hivyo pande zote mbili zimeshtumiana kukiuka usitishwaji huo wa mapigano kwa saa 30, Ukraine ikisema Urusi ilishambulia kwa droni na makombora maeneo ya Dnipropetrovsk na Mykolaiv.
Hata hivyo Moscow imekanusha taarifa hiyo na kueleza kuwa vikosi vyake viliheshimu kikamilifu hatua hiyo iliyochukuliwa na rais Vladimir Putin.
Aidha, Msemaji wa wizara ya mambo ya Nje wa China Guo Jiankun amepongeza juhudi zote zinazo chukuliwa ili kufikia usitishaji mapigano nchini Ukraine, akisisitiza kuwa ni hatua muhimu kuelekea amani.