1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yachukuwa udhibiti wa maeneo mawili ya makazi Ukraine

19 Januari 2026

Vikosi vya Urusi vimechukua udhibiti wa eneo la makazi la Pavlivka, katika eneo la Zaporizhzhia nchini Ukraine na Novopavlivka mkoani Donetsk. Haya yamesemwa leo na wizara ya ulinzi ya Urusi.

Kherson 2026 | Shambulizi la Urusi
Shambulizi la Urusi dhidi ya hoteli moja nchini Ukraine mnamo Januari 1, 2026 katika eneo la KhersonPicha: Vladimir Saldo/Telegram/REUTERS

Ripoti hiyo ya Urusi ya kuteka maeneo mawili ya Ukraine haikuweza kuthibitishwa na Reuters kwa njia huru.

Urusi yashambulia kituo cha miundo mbinu Kharkhiv

Meya wa Kharkiv Ihor Terekhov, amesema leo kuwa kituo kimoja muhimu cha miundombinu kimeharibiwa mjini humo kutokana na shambulizi la Urusi.

Kwenye ujumbe katika mtandao wa Telegram, Terekhov amesema adui alishambulia kituo hicho kwa makombora kadhaa na kusababisha uharibifu mkubwa. Hata hivyo hakutoa maelezo yoyote kuhusu aina ya kituo kilichoshambuliwa.

Katika hatua nyingine, wafanyakazi wa ukarabati wa dharura wanafanya kazi kwa bidii ili kurejesha nguvu za umeme mkoani Kyiv nchini Ukraine, baada ya mfululizo wa mashambulizi ya Urusi dhidi ya miundombinu ya nishati kuwaacha raia wa eneo hilo kwenye kibaridi kikali cha msimu wa huu wa baridi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW