1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi yadungua droni iliokuwa inakaribia mji wa Moscow

31 Agosti 2023

Walinzi wa anga nchini Urusi wameharibu ndege isiyoendeshwa na rubani au droni,iliyokuwa ikikaribia kufika mjini Moscow.

Drohnenangriff auf Moskau
Picha: Mikhail Tereshchenko/ITAR-TASS/IMAGO

Hayo yameelezwa na meya  wa Moscow Sergei Sobyanin kupitia ujumbe aliouandika kwenye ukurasa wa mtandao wa Telegram leo Alhamisi.

Amesema wanajeshi wa ulinzi wa angakatika wilaya ya Voskresensky iliyoko takriban kilomita 60 kutoka Moscow waliiharibu droni hiyo iliyokuwa ikielekea Moscow, japo hakusema wapi ilikotokea.

Soma pia:Mashambulizi ya droni ya Ukraine dhidi ya Moscow yanaweza kuongezeka

Hata hivyo baadae wizara ya ulinzi ya Urusi ilitowa taarifa ikisema ndege hiyo ilikuwa ya Ukraine.

Hakuna kifo wala uharibifu uliosababishwa na tukio hilo kwa mujibu wa meya na watoa huduma za dharura wapo katika eneo la tukio.

Jana maeneo mengi ya Urusi yalilengwa na mashambulizi makubwa  ya Usiku ikiwemo uwanja wa ndege wa Pskov ulioko karibu na mpaka wa Estonia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW