1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yafanya mashambulizi makubwa nchini Ukraine

20 Septemba 2025

Urusi mapema leo Jumamosi imefanya mashambulizi makubwa ya makombora na droni yaliolenga maeneo mbali mbali kote nchini Ukraine na kuwauwa takriban watu watatu na kuwajeruhi mamia ya wengine .

Ufaransa Paris 2025 | Mkutano na Rais Macron
Rais wa Ukraine, Volodymyr ZelenskyPicha: Julien Mattia/Le Pictorium/MAXPPP/picture alliance

Katika taarifa kupitia mtandao wake rasmi wa Telegram, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy, amesema mashambulizi hayo yamefanyika katika mikoa tisa ikiwa ni pamoja na Dnipropetrovsk, Mykolaiv, Chernihiv, Zaporizhzhia, Poltava, Kyiv, Odesa, Sumy na Kharkiv.

Rais huyo amesema lengo la kile alichokiita adui ni miundombinu yao, maeneo ya makazi na makampuni ya kibiashara ya raia.

Pia amesema kombora moja lililenga jengo la ghorofa nyingi katika jiji la Dnipro.

Rais Zelensky ameongeza kuwa kila shambulizi sio shabaa ya kijeshi lakini ni mkakati wa makusudi wa Urusi kuwatisha raia na kuharibu miundombinu yao.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW