Urusi yafanya mashambulizi makubwa nchini Ukraine
18 Mei 2026
Hayo yameelezwa na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na kuongeza kuwa Urusi ilifyetua jumla ya makombora 22 ya masafa na droni 524.
Kwa siku kadhaa sasa, Moscow imekuwa ikijibu mashambulizi makubwa zaidi ya droni yaliyofanywa na Ukraine na kusababisha vifo vya watu wasiopungua wanne, wakiwemo watatu karibu na Moscow. Wiki iliyopita, shambulio la Urusi lilibomoa jengo la ghorofa mjini Kyiv ambapo watu 24 waliuawa.
Hadi sasa , hakuna ishara ya kufikiwa kwa makubaliano ya amani licha ya juhudi za kidiplomasia zinazoongozwa na Marekani kujaribu kukomesha uvamizi huo. Hayo yanaripotiwa wakati rais wa Urusi Vladimir Putin anatarajiwa kuanza hapo kesho ziara yake nchini China na anatarajiwa kukutana na mwenzake Xi Jinping, ikiwa ni siku chache baada ya ziara ya rais wa Marekani Donald Trump mjini Beijing.