Urusi yafanya shambulizi dhidi ya gridi ya umeme ya Ukraine
20 Januari 2026
Matangazo
Meya wa Kyiv, Vitali Klitschko amesema shambulizi hilo lilisababisha kukatika kwa umeme katika zaidi ya majengo 5,600 ya ghorofa kwenye mji huo mkuu.
Takriban asilimia 80 ya majengo yaliyoathiriwa yalikuwa yamerejeshewa umeme hivi karibuni baada ya shambulizi kubwa la Urusi mnamo Januari 9 lililowaathiri maelfu ya watu kwa siku kadhaa.
Wakati huo huo, maafisa wa Ukraine wanajaribu kuendeleza kasi ya mazungumzo ya amani yanayoongozwa na Marekani. Timu yake ya mazungumzo iliwasili Marekani siku ya Jumamosi. Kwa mujibu wa Zelensky, jukumu lake kuu ni kueleza jinsi mashambulizi ya Urusi yanahujumu diplomasia.