1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yaishambulia tena Kiev kwa droni

30 Septemba 2024

Urusi imefanya mashambulizi ya droni mapema leo katika mji mkuu wa Ukraine, Kiev, huku jeshi la Ukraine likisema vitengo vyote vya mifumo ya ulinzi wa anga wa makombora viliingia kazini kuyazuia mashambulizi hayo.

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine.
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine.Picha: Ukraine Presidency/Planet Pix/Zuma/picture alliance

Mji wa Kiev na viunga vyake na eneo zima la mashariki mwa Ukraine yamewekwa katika hali ya tahadhari ya kushambuliwa kutokea angani.

Haya yanajiri siku moja baada ya Ukraine kuishambulia Urusi kwa droni zaidi ya 100 ambapo ghala kubwa la silaha lilishambuliwa, pamoja na maeneo ya ndani zaidi nchini Urusi.  

Soma zaidi: Urusi yaushambulia mji wa Kiev kwa droni

Siku ya Jumatatu (Septemba 30), Rais Vladimir Putin wa Urusi alisema kwamba nchi yake itatimiza malengo yake yote ya vita dhidi ya Ukraine, huku vita hivyo vikiwa vinaingia katika mwaka wa tatu.

Wakati huo huo, Denmark imetangaza msaada wa dola milioni 194 wa kuisadia Ukraine inapokabiliana na uvamizi wa Urusi. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW