1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yakataa kupangiwa na EU kusitisha vita Ukraine

12 Mei 2025

Urusi imesema Umoja wa Ulaya haupaswi kuipangia muda wa kusitisha vita Ukraine, ikisisitiza kuwa maamuzi kuhusu mzozo huo yanapaswa kufikiwa kupitia mazungumzo ya moja kwa moja na kuzingatia maslahi ya pande zote.

Rais wa Urusi Vladmir
Rais wa Urusi VladmirPicha: Newen

Urusi imesema haiwezi kukubali kupewa muda wa mwisho na Umoja wa Ulaya  kusitisha vita nchini Ukraine.

Tamko hilo la Kremlin limetolewa baada ya viongozi wa Umoja wa Ulaya kuitaka Urusi ikubali,kufikia leo usiku, pendekezo la kusitisha vita kwa siku 30.Soma pia: Viongozi wa Ulaya wakutana London kuujadili mzozo wa Ukraine

Mawaziri wa mambo ya nje kutoka Ufaransa,Italia,Ujerumani,Uhispania, Poland na Umoja wa Ulaya wanakutana mjini London na mwenyeji wao David Lammy,waziri wa mambo ya nje wa Uingereza, kujadili hatua za kuchukuwa dhidi ya Urusi.

Lammy anatarajiwa kutangaza vikwazo zaidi vitakavyowalenga washirika wa Urusi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW