Urusi yasema Ukraine imeshambulia meli yake Libya
4 Machi 2026
Matangazo
Mamlaka ya bandari ya Libya imesema meli hiyo ya mizigo ya Urusi, Arctic Metagaz, ilizama baada ya "milipuko ya ghafla" kaskazini mwa bandari ya Sirte.
Pia imesema meli hiyo ilikumbwa na milipuko ya ghafla iliyofuatiwa na moto mkubwa, ambao hatimaye ulisababisha kuzama kwake kabisa.
Moscow pia imesema meli hiyo ya mafuta ilishambuliwa na droni za Ukraine kutoka pwani ya Libya katika "kitendo cha ugaidi wa kimataifa na uharamia wa baharini".
Pia imesema abiria wote 30 wameokolewa.
Meli hiyo ilikuwa imewekewa vikwazo na Marekani na Umoja wa Ulaya.