Urusi yashambulia gridi ya umeme nchini Ukraine
7 Februari 2026
Matangazo
Katika ujumbe kwenye mtandao wa telegram, kampuni hiyo imesema mashambulizi hayo bado yanaendelea lakini shughuli ya urekebishaji itaanza mara tu hali ya usalama itakapoimarika.
Waziri Mkuu wa Ukraine Denys Shmygal amesema nchi hiyo imeomba msaada wa dharura kutoka Poland baada ya shambulizi la Urusi dhidi ya vinu vya kuzalisha umeme vya Burshtynska na Dobrotvirska magharibi mwa Ukraine.
Maafisa nchini Ukraine wameishutumu Moscow kwa kulenga miundombinu ya nishati kimakusudi, na kusababisha kukatika kwa umeme ambako kumewaacha mamia ya maelfu ya watu bila umeme wakati wa msimu huu mkali wa baridi.